Swalah ya Kuomba Mvua
SWALAH YA KUOM BA MVUA Taarif (Maana ) yake “Al-Istisqaa” ni kumwomba Allaah Aiteremshe mvua wakati wa ukame. Maulamaa wote wamekubaliana kwamba hilo ni Sunnah aliyoiweka Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihiy wa sallam), lakini wamekhitalifiana kuhusiana na Swalaah yenyewe kama tutakavyobainisha. Hukmu ya Swalaah ya Kuomba Mpya Ukame ukiingia, ardhi ikakauka na mvua ikapotea, imesuniwa imamu atoke pamoja na watu hadi sehemu maalumu ya kuswalia kama tutakavyoeleza, kisha aswali nao rakaa mbili. Hili ndilo lililothibiti toka kwa Nabiy wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Imepokelewa toka kwa ‘Abbaad bin Tamiym toka kwa ami yake akisema: “Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitoka kwenda sehemu ya kuswalia kwa ajili ya kuomba mvua. Alielekea Qiblah na kuswali rakaa mbili na akageuza nguo yake kwa kupindua kulia kuja kushoto.” [ Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy]. ...