Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2021

Adabu za Ndoa

 Adabu za Ndoa katika Sunnah MKE NA MUME KUOGA PAMOJA Inaruhusiwa kwa mume na mke kukoga pamoja katika sehemu moja hata  kama  mume ataona sehemu za siri za mke na mke ataona sehemu za siri za mumewe. Hii imethibitika katika Hadiyth Swahiyh mbali mbali, miongoni mwa hizo ni:   Kwanza :   عَنْ عَائِشَة ، قَالَتْ: كُنْتُ أَغْتَسِلُ أَنَا وَرَسُولُ اللّهِ مِنْ إِنَاءٍ. ـ بَيْنِي وَبَيْنَهُ ـ، وَاحِدٍ (تختلف أيدينا فيه). فَيُبَادِرُنِي حَتَّى أَقُولُ: دَعْ لِي، دَعْ لِي. قَالَتْ: وَهُمَا جُنُبَانِ   Imetoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah  رضي الله عنها  ambaye alisema: "Nilikuwa nakoga na Mtume kutoka chombo kimoja cha maji kilichowekwa baina yetu (kiasi kwamba mikono yetu ilikuwa ikipishana katika maji). Alikuwa akishindana na mimi hadi nikasema: Nibakishie (maji), nibakishie (maji)". Akaongeza: "Tulikuwa katika hali ya janaba"  (yaani hali ya kutoka katika tendo la ndoa ) Imepokelewa na Imaam Al-Bukhaariy na Muslim  Pili:   عن معاوية بن...

Eda: Maana ya Eda, Hikma ya Eda , Hukmu zake, Mambo yanayopasa na uyasiyopasa kwa mwenye Eda

  Maana ya Eda, Hikma ya Eda , Hukmu zake, Mambo yanayopasa na uyasiyopasa kwa mwenye Eda Assallaam Aleykum Warahmatullaah Wabarakatuh Maana ya Eda Eda ni kipindi anachokaa mwanamke aliyeachika (Talaka) au aliyefiwa na mumewe, na baada ya kipindi hicho ndoa yake huwa halali. Na imeitwa eda kwa jina hili kutokana na jina la kiarabu ‘ iddah ’ kwa kukusanya kwake (idadi) ya miezi au quruu au au hedhi au vipindi vya tohara ya hedhi. Maana ya Quruu Kuna kutofautiana kwa maoni ya ‘Ulamaa kuhusu hii quruu, je, ni Twahara au ni hedhi?   Quruu , ni neno linalotumika kwa maana ya hedhi au Twahara kwa vile linaoana na maana zote mbili. Hanafiy na Hanbaliy, wanaona kwamba neno hili lina maana ya hedhi. Hii inamaanisha kwamba mwanamke aliyeachwa atakaa hadi hedhi tatu zimalizike. Ikiwa hedhi itakatika baada ya mara moja tu, basi itakamilishwa na miezi. Ama Imaam Maalik na Ash-Shaafi'iyy, wao wanaona kwamba neno hili lina maana ya Twahara. Na Twahara hapa ni vile vipindi vinavyokuw...

Tuache Kufuata Matamanio

           Tuache Kufuata Matamanio   Assallaam Aleykum Warahmatullaah Wabarakatuh Enyi Waislamu muogopeni Allaah kwa kadri Anavyopaswa kuogopewa. Allaah Amesema,   يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ   ﴿١٠٢﴾   Enyi walioamini! Mcheni Allaah kama ipasavyo kumcha na wala msife isipokuwa nyinyi (mmeshakuwa) ni Waislamu .  [Aal 'Imraan:102]   Uchaji Allaah ni dalili ya iymaan. Kwani kwa uchaji Allaah ndipo mtu anaweza kudumu katika njia iliyonyooka (iliyo sawa).   Jueni kuwa muongozo sahihi ni muongozo wa Muhammad (Swalla Allahu ‘alayhi wa sallam), Ubaya wa mambo yote ni uzushi, na kila uzushi ni uovu, na kila ovu linampeleka mtu motoni.   Enyi Waislamu! Allaah Amewaumba viume ili wamuabudu na wafungamane na Amri Zake na makatazo Yake. Allaah Anasema, وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ ﴿٥٦﴾   Na Sikuumba ma...

Mambo yanayomtoa Mtu katika Uislaam

  Mambo yanayomtoa Mtu katika Uislaam Assallaam Aleykum Warahmatullaah Wabarakatu Naam tambua ya kwamba mambo yanayomtoa Muislamu katika Uislamu ni mambo kumi, ambayo ni kama yafuatayo;   Moja:  Ni kumshirikisha Allaah Aliyetukuka katika ibada, Anasema Allaah:     إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا   ﴿١١٦ Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini  amepotoka upotofu wa mbali.   [An-Nisaa: 116]   Na Anasema Allaah:  ۖإِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni motoni. Na madhalimu hawatopata yeyote mwenye kunusuru.   [...

Faida za Kuacha Elimu Duniani

  Thawabu zako ukiwa hai na baada ya kufa Miongoni mwa matunda ya elimu ni ule uendeleaji wa thawabu katika uhai na baada ya kufa. Mwanafunzi anapojifunza elimu kisha akaieneza kwa muislamu ambapo muislamu huyu akatendea kazi elimu hii, anakuwa na ujira mkubwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema: “Atayejifunza elimu ana ujira wa yule atayaitendea kazi. Hakutopungua kitu katika ujira wa yule mtendaji.” Ibn Maajah (240). al-Albaaniy amesema katika “Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb” (01/19): “Ni Swahiyh kutokana na zengine.” Mwanafunzi! Pindi utapojifunza Sunnah, faradhi au Dhikr kisha ukamfunza muislamu ambapo muislamu huyo akaja kutendea kazi kitu hicho, basi utakuwa na ujira mfano wa ujira wake. Na muislamu huyo akimfunza mwingine, wewe bado utapata sawa na ujira wa yule mtu mwingine. Hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah! Ninaapa kwa Allaah ya kwamba hizi ni thawabu na ujira mwingi. Uhakika wa mambo ni kuwa ujira hausimami kwa wewe kufa. Bado utaendelea kupata ujira i...

Fadhila za kujifunza Elimu ya Dini

  Fadhila za kujifunza Elimu ya Dini Kumekuja dalili nyingi zenye kubainisha fadhila za elimu ili kutia hamu na kuzivutia nafsi kupata jambo hilo kubwa. Allaah (´Azza wa Jall) amesema: إِنَّمَا يَخْشَى اللَّـهَ مِنْ عِبَادِهِ الْعُلَمَاءُ “Hakika wanaomkhofu Allaah kihakika miongoni mwa waja Wake ni wasomi.” 40:28 Hakika wale ambao wanamcha Allaah ukweli wa kumcha ni wanachuoni. Wanachuoni woga wao wa kumuogopa Allaah ni mkamilifu. Kwa kuwa maarifa yao ya kumjua Allaah ni kamilifu. Allaah (´Azza wa Jalla) amesema: يَرْفَعِ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ وَالَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ دَرَجَاتٍ “Allaah atawainua wale walioamini miongoni mwenu na waliopewa elimu daraja za juu zaidi.” 58:11 Wale ambao Allaah (´Azza wa Jall) kwanza amewaruzuku imani, kisha akawaruzuku pamoja na imani elimu, basi Allaah (´Azza wa Jall) atawanyanyua daraja za juu duniani na Aakhirah. Wao ndio wako juu na wenye kustahiku kusifiwa na walio na ujira mkubwa. Hapa kuna dalili kubwa ya kwamba elimu katika U...