Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2021

Fisadi Gani Mbili za Mayahudi zilizotajwa katika Suwrat Bani Israaiyl?

  SWALI:   Assalam alaykum Natumai mnaendelea vizuri na afya njema na shughuli zenu za Dawa. Ningependa kuuliza: Katika kitabu kitukufu Qur'an, Allaah ameelezea katika Suwrah Al-Israa au Bani Israel katika aayah ya 4 - 5. Napenda kujua hizo fisadi mbili zilizoandikwa kuwa Wana wa Israel watazifanya, haswa hiyo ya kwanza ilitokea wakati gani na wakati wa Nabiy gani. Na ni watu gani katika waja wake Allaah ambao aliwapeleka kuwatia adabu. Kisha napenda kujua hiyo fisadi ya pili ni ipi au lini itatokea. Na kama kuna mengine ya ziada tuchambulini kwa hawa watu ambao Allaah amewalaani kwa jeuri yao. Shukran   JAWABU: Hakika hili ni swali nyeti ambalo inatakiwa kila Muislamu awe na ufahamu nalo. Swala la Mayahudi ambao Qur-aan, Hadiyth za Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na hata historia imetubainishia uovu wao usio kifani. Lakini hapa si mahali pake kuelezea hayo kwani swali mbele yetu ni jengine japokuwa linahusiana.     Hakika ufisadi wa...

Je, بسم الله (BismiLLaah) Inahesabika Kuwa Ni Aayah Katika Suwratul Faatihah?

  Je,  بسم الله (BismiLLaah)  Inahesabika Kuwa Ni Aayah Katika Suwratul Faatihah? JAWABU: Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu Bismillaahi ar-Rahmanir Rahiym katika Suwrah Faatihah na Suwrah nyinginezo. Kuhusu suala hilo kuna tofauti baina ya wanachuoni na kila mmoja ana dalili zake kuhusu hilo:   Mwanzo ni kuwa wanazuoni wamekubaliana kuwa al-basmalah (BismiLlaahir Rahmaanir Rahiym) iliyopo katika Surawh Naml (27) kuwa ni sehemu ya Aayah katika kauli Yake Aliyetukuka:   إِنَّهُ مِن سُلَيْمَانَ وَإِنَّهُ بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ ﴿٣٠﴾ 30. Hakika hiyo ni kutoka kwa Sulaymaan, na hakika hiyo (imeanza) Kwa Jina la Allaah, Ar-Rahmaan, Mwenye kurehemu. [An-Naml: 30]   Na haihesabiwi kuwa ni mwanzo wa Aayah ya Suwrah hiyo, na kuisoma mwanzo wa Suwrah hiyo ni Makruuh.   Hata hivyo, wanachuoni wametofautiana kama al-basmalah ni Aayah katika Suwrah Faatihah na katika mwanzo wa kila Suwrah au la? Kauli za wanachuoni katika hilo ni kama zif...

Mwanamke mwenye hedhi kusoma vitabu vya dini

  Swali:  Inajuzu kwangu kwa mfano kusoma vitabu kama “Fiqh-us-Sunnah” au vitabu vyengine vya dini wakati niko na hedhi? Jibu:  Inajuzu kwa mwanamke mwenye hedhi kumdhukuru Allaah, kusema “Subhaan Allaah”, kusema “Laa ilaaha illa Allaah”, kusema “Allaahu Akbar” na asome vitabu vya dini atakavyo.  Ni mamoja vitabu hivi ni vya tafsiri ya Qur-aan, Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), vya Fiqh au vyenginevyo.  Hakuna neno juu yake kwa kufanya hivo. Kuhusu kusoma Qur-aan akiwa na hedhi ni jambo ambalo wanachuoni wametofautiana.  Lakini maoni tunayoona kuwa yana nguvu ni kwamba si haramu kwake kusoma Qur-aan akihitajia kufanya hivo.  Kwa mfano ni mwalimu wa kike na anahitajia kusoma Qur-aan mbele ya wanafunzi wa kike kwa ajili ya mafunzo, akawa ni mwanafunzi wa kike na anahitajia kusoma Qur-aan kwa ajili ya mitihani au mfano wa hayo, katika hali hizi hakuna neno.  Kwa sababu, kama alivyosema Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaa...

Mwenye Hedhi kuingia Msikitini na Hukmu ya Kupata Hedhi mara mbili ndani ya mwezi mmoja?

  *Swali* A ssalam Alleykum je inajuzu mwanamke mwenye hedhi kuingia msikitini kwa ajili ya kusoma ?? je nikipimo gani kishilia kutenganisha dam ya hedhi na homa au ni masiku mangapi kwa mwanamke yakipita utasema dam hii ni hedhi na sasa ni homa akaswali na kusoma quani ?? au mwanamke kupata hedhi mala mbili kwa mwezi mmoja nini jukum yake ?? *Jawabu* Wa Aleykum Salaam WarahmatulLaah Wabarakatuh... ✅Naam nakumbuka katika Kitaab Fiqh'i Sunnah-Mlango wa Twahara nilielezea kwa Mapana sana kuhusiana na Masuala ya Damu ya Hedhi na Hukmu zake.. ➡️Kwa kifupi sana Ni damu nyeusi, nzito na yenye harufu mbaya. Inamtoka mwanamke toka sehemu maalumu katika nyakati maalumu. ➡️Damu ya hedhi haina mpaka wa uchache wala wingi, bali hilo linategemea maumbile ya mwanamke, kwa vile hakuna dalili yoyote sahihi toka kwa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inayobainisha uchache wake au wingi wake. Kwahiyo Damu ya Hedhi inaweza ikakatika kwa siku 1 au 2 au 4 na wengine hadi siku 7...