Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2021

Kuinunua na Kuisafirisha Zakaah

 KUINUNUA NA KUISAFIRISHA ZAKAAH Mtume Muhammad (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) amekataza mtu kuinunua Zakaah yake.  Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Llaahu ‘anhu), amesema:   "‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alimtoa farasi wake Swadaqah fiy sabiyli Llaah, kisha akamkuta farasi huyo anauzwa na akataka kumnunua. Akamuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya jambo hilo, akamwambia:   "Usimnunue na wala usirudie (kutaka kuimiliki tena) Swadaqah yako"  [ Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo]   Baadhi ya maulamaa wakasema kuwa kukataza huko ni kwa ajili ya kujiepusha tu, na si kwa ajili ya kuharamisha, wakiegemea Hadiythi nyingine inayoruhusu mtu kuipokea Swadaqah yake kama zawadi itokayo kwa masikini aliyempa. Hukmu  ya Kuisafirisha Zakaah ‘U lamaa wengi wamekubali kuwa mali ya Zakaah (Zakaatul Maal - si Zakaatul Fitwr) inaweza kusafirishwa na kutolewa katika nchi nyingine kwa wanaoistahiki z...

Watu Wema Kupewa Zakaah

 WATU WEMA KUPEWA ZAKAAH Zakaah anapewa Muislam anayeistahiki akiwa Muislam huyo ni mtu mwema au mtu asi, isipokuwa mtu asi hapewi katika mali ya Zakaah ikiwa itajulikana kwa uhakika kuwa atakuja kuitumia mali hiyo katika kuuendeleza uasi wake.   Ikijulikana kwa uhakika kuwa ataitumia mali hiyo katika kumuasi Allaah, basi mtu huyo atanyimwa, ama ikiwa hayajulikani hayo, au ikijulikana kuwa ataitumia mali hiyo katika shida zake, basi hapo atapewa.   Hata hivyo ni bora kwa mtoaji Zakaah aihusishe mali hiyo kwa kuwapa watu wema au maulamaa wanaostahiki wanaoifayia kazi elimu yao, kwani Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:   "Walisheni chakula chenu waja wa Allaah na mnaowajuwa katika walioamini (kweli)".   [Ahmad]   Anasema Ibn Taymiyah:   "Asiyeswali hapewi katika mali ya Zakaah mpaka pale atakapotubu akawa anaswali."   Anasema Sayyid Saabiq:   "Kat...

Watu ambao ni Haramu kupewa Zakaah

 WALIOHARAMISHWA KUPEWA ZAKAAH Naam wafuatao ni Watu ambao ni Haramu kupewa Zakaah... 1.    Kafiri   Katika Hadiyth iliyotangulia, Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:   "Zichukuliwe kutoka kwa matajiri Wao na kurejeshewa masikini Wao"    Na maana yake ni kuwa:-   Zichukuliwe kutoka kwa matajiri wa Kiislam na kupewa masikini wa Kiislam.     2.    Bani Hashim   Nao ni watoto wa Aliy na Aqiyl na Jaafar na Al ‘Abbaas na Al Harith (Radhwiya Allaahu ‘anhum).   Nabiy (Swalla Llaahu ‘alayhi wa sallam) amesema:   "Swadaqah haijuzu kupewa kwa watu wa Muhammad".  [ Muslim]   ‘Ulamaa wamekhatalifiana juu ya ukoo wa Bani Al Muttalib, iwapo nao pia hawapewi katika mali ya Zakaah au wanapewa.   Imaam Ash-Shaafi’iy amesema kuwa hawa nao wasipewe katika mali ya Zakaah, na hii inatokana na Hadiyth  iliyotolewa na Imaam Ash-Shaafi’iy na Imaam Ahmad ...

Wanaotakiwa Kupewa Zakaah

 WANAOSTAHIKI KUPEWA ZAKAAH  Swadaqah ya kawaida, anapewa mtu yeyote hata akiwa si Muislam, ama Zakaatul Fitwr wanapewa watu wa aina mbili tu, nao ni masikini na mafakiri Waislam. Zakaatul Maal (Zakaah ya mali), hii wanapewa aina 8 tu ya Waislamu waliowataja na Allaah katika kitabu chake kitukufu Aliposema:   إِنَّمَا الصَّدَقَاتُ لِلْفُقَرَاء وَالْمَسَاكِينِ وَالْعَامِلِينَ عَلَيْهَا وَالْمُؤَلَّفَةِ قُلُوبُهُمْ وَفِي الرِّقَابِ وَالْغَارِمِينَ وَفِي سَبِيلِ اللّهِ وَابْنِ السَّبِيلِ فَرِيضَةً مِّنَ اللّهِ وَاللّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ     "Swadaqah hupewa (watu hawa):- 1. Mafakiri na 2. Masikini na 3. Wanaozitumikia na 4. Wanaotiwa nguvu nyoyo zao (juu ya Uislam) na 5. Katika kuwapa uungwana watumwa na 6. Katika kuwasaidia Wenye deni na 7. Katika (kutengeneza) Mambo aliyoamrisha Allaah na 8. Katika (kupewa) Wasafiri (walioharibikiwa).  ۖ فَرِيضَةً مِّنَ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ Ni faradhi itok...

Zakaatul Fitwir na Hukmu zake

 ZAKAATUL FITWIR NA HUKMU ZAKE   Imefaridhishwa katika mwezi wa Sha'abani mwaka wa 2 baada ya Hijrah (baada ya kuhamia Madiynah). Rasuli wa wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alifaridhisha Zakaatul Fitwr ili iitakase saumu kutokana na dhambi ndogo ndogo zilizopatikana ndani ya mazungumzo na matendo. Na wakati huo huo Zakaah hiyo iwe msaada kwa mafakiri na wasiojiweza katika kuisherehekea Sikukuu.     Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kuwa amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alifaridhisha Zakaah ya Fitwr kwa ajili ya kumtakasa aliyefunga kutokana na dhambi ndogo ndogo za mazungumzo na matendo, na ili wafaidike masikini. Atakayeitoa kabla ya Swalaah (ya 'Iyd) inakubaliwa kama Zakaah ya Fitwr na atakayeitoa baada ya Swalaah inakubaliwa kama Swadaqah ya kawaida."  [Abuu Daawuwd – Ibn Maajah na Ad-Daaraqutniy]   Alikuwa (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akitoa Zakaah ya ...

Swadakah na Fadhila Zake

 KUTOA SWADAQAH  Swadaqah Muislam anaipa mali yake mtazamo wa aina nyingine kabisa tofauti na asiyekuwa Muislam, kwani dini ya Kiislam inampa kila mtu haki ya kutafuta mali na kufanya biashara ya halali na kuwa tajiri anayeweza kumiliki mali nyingi.  Isipokuwa baada ya kuimiliki mali hiyo, analazimika kuwapa maskini Zakaah, ambayo ni haki yao maalum waliyopangiwa na Mola wao Subhanaahu wa Ta’aalaa.   Wakati huo huo Muislam anatakiwa ajipatie thawabu nyingi zaidi na ajiepushe na shari nyingi pamoja na kuwasaidia ndugu na jamaa zake, na masikini waislamu wenzake wenye kuhitaji, kwa kutoa kiasi kingine katika mali zao kwa hiari yao wenyewe na kwa kiasi anachokitaka mwenyewe, na hii inaitwa 'Swadaqah'.   Kinyume na njia inayotumika katika nchi za Kikoministi za kuwanyang'anya matajiri mali zao kwa nguvu na kuwapa masikini, kitendo cha dhulma na cha ufisadi, kwa sababu binaadamu kwa kawaida wanakhitalifiana katika ujuzi na katika jitihada zao, na kwa ajili hiyo lazim...

Zakaah ya Madini ya kale

  Zakaah Ya Madini Ya Kale   Madini inayotolewa ardhini kama vile petroli, gesi, shaba, chuma n.k, hivi vyote havitolewi Zakaah, isipokuwa dhahabu na fedha tu na tushaelezea hapo mwanzo namna ya kutoa Zakaah yake.  Ama vilivyobaki vinatolewa Zakaah ya biashara baada ya kuchimbuliwa au kutolewa na kuuzwa. Na Allaah anajua zaidi 

Zakaah ya Wanyama Wanaofugwa

 ZAKAAH YA WANYAMA WANAOFUGWA Wanyama wanaofugwa wanalazimika kutolewa Zakaah kwa masharti yafuatayo: 1.  Lazima watimie Niswaab 2.  Wakamilishe mwaka 3.  Wawe wanyama wa kufugwa.   Wanyama wasiokuwa wa kufugwa kama vile wa kupandwa au wanaotumiwa kwa kubeba mizigo au kwa kilimo n.k. Hawa hawatolewi Zakaah. Wanyama wanaotolewa Zakaah ni Ngamia, Ng'ombe, Mbuzi na Kondoo.   Zakaah ya Ngamia   Ngamia hawatolewi Zakaah mpaka watimie watano. Wakitimia watano wa kufugwa hadi tisa na kutimiza mwaka chini ya milki ya mtu, basi atawatolea mbuzi mmoja.   Wakitimia ngamia 10 mpaka 14 atawatolea mbuzi wawili.   Na hivyo hivyo kila wakizidi ngamia watano ataongeza mbuzi mmoja. Wakitimia ngamia 25 mpaka 35 atatoa mtoto wa ngamia jike aliyekamilisha mwaka na kuingia mwaka wa pili au mtoto wa ngamia dume aliyekamilisha mwaka wa 2 na anaingia wa 3.   Kuanzia ngamia 36 mpaka 45 atatoa mtoto wa ngamia jike aliyekamilisha miaka 2 na keshaingi...

Zakaah ya Mazao

 ZAKAAH YA MAZAO Allaah Amewajibisha kuyatolea Zakaah mazao Aliposema:   وَهُوَ الَّذِي أَنشَأَ جَنَّاتٍ مَّعْرُوشَاتٍ وَغَيْرَ مَعْرُوشَاتٍ وَالنَّخْلَ وَالزَّرْعَ مُخْتَلِفًا أُكُلُهُ وَالزَّيْتُونَ وَالرُّمَّانَ مُتَشَابِهًا وَغَيْرَ مُتَشَابِهٍ كُلُواْ مِن ثَمَرِهِ إِذَا أَثْمَرَ وَآتُواْ حَقَّهُ يَوْمَ حَصَادِهِ Naye (Allaah) Ndiye Ambaye Aliyezalisha mabustani yanayotambaa na yasiyotambaa. Na mitende na mimea yakitofautiana kwa ladha yake, na zaytuni na makomamanga yanayoshabihiana na yasiyoshabihiana. Kuleni katika matunda yake yanapotoa mazao na toeni haki yake (Zakaah) siku ya kuvunwa kwake.  [Al-An’aam: 141]   Katika kuifasiri Aayah hii amesema Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhu):   'Haki yake, ni Zakaah yake iliyofaradhishwa".   Wakati wa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Zakaah ya mazao ilikuwa ikitolewa katika Mahindi, Ngano, Mtama, Tende na Zabibu na wengine wakaongeza 'Mchele' na wengine wakasema kuwa Zakaah ya maz...