Picha ya Namna ya Kuswali swalah ya Kupatwa kwa Jua/Mwezi
Picha ya Swalaah ya Kusuwf Kwa Muhtasari
1- Apige takbiyr, asome du’aa ya ufunguzi, asome isti’aadhah, asome Al-Faatihahh, na kisha asome kiasi cha Suwrat Al-Baqarah.
2- Arukuu rukuu ndefu.
3- Anyanyuke toka kwenye rukuu na aseme: “Sami’a Allaahu liman hamidahu, Rabbanaa walakal Hamdu”.
4- Asisujudu, bali asome Al-Faatihah na Suwrah fupi kidogo kuliko ile ya kwanza.
5- Arukuu tena rukuu ndefu na apunguze kidogo urefu kulinganisha na ile ya kwanza.
6- Anyanyuke toka kwenye rukuu na aseme: “Sami’a Allaahu liman hamidahu, Rabbanaa walakal Hamdu”.
7- Asujudu, kisha akae, halafu asujudu tena.
8- Anyanyuke kwenda rakaa ya pili, kisha afanye kama alivyofanya katika rakaa ya kwanza.
Inaendelea.....
Na Allaah anajua zaidi
Maoni
Chapisha Maoni