Picha ya Namna ya Kuswali swalah ya Kupatwa kwa Jua/Mwezi

Picha ya Swalaah ya Kusuwf Kwa Muhtasari

 

1- Apige takbiyr, asome du’aa ya ufunguzi, asome isti’aadhah, asome Al-Faatihahh, na kisha asome kiasi cha Suwrat Al-Baqarah.

 

2- Arukuu rukuu ndefu.

 

3- Anyanyuke toka kwenye rukuu na aseme: “Sami’a Allaahu liman hamidahu, Rabbanaa walakal Hamdu”.

 

4- Asisujudu, bali asome Al-Faatihah na Suwrah fupi kidogo kuliko ile ya kwanza.

 

5- Arukuu tena rukuu ndefu na apunguze kidogo urefu kulinganisha na ile ya kwanza.

 

6- Anyanyuke toka kwenye rukuu na aseme: “Sami’a Allaahu liman hamidahu, Rabbanaa walakal Hamdu”.

 

7- Asujudu, kisha akae, halafu asujudu tena.

 

8- Anyanyuke kwenda rakaa ya pili, kisha afanye kama alivyofanya katika rakaa ya kwanza.


Inaendelea.....


Na Allaah anajua zaidi 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Eda: Maana ya Eda, Hikma ya Eda , Hukmu zake, Mambo yanayopasa na uyasiyopasa kwa mwenye Eda

Namna ya Kuswali Swalat Kusuwf (Swalah ya Kupatwa kwa Jua/Mwezi

Ramadhwaan ni Mwezi wa Du’aa na Du’aa hutakabaliwa